_id
stringlengths
15
22
url
stringlengths
31
150
title
stringlengths
1
86
text
stringlengths
100
23.8k
20231101.sw_2_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Akiolojia (kutoka Kiyunani αρχαίος = zamani na λόγος = neno, usemi) ni somo linalohusu mabaki ya tamaduni za watu wa nyakati zilizopita. Wanaakiolojia wanatafuta vitu vilivyobaki, kwa mfano kwa kuchimba ardhi na kutafuta mabaki ya majengo, makaburi, silaha, vifaa, vyombo na mifupa ya watu.
20231101.sw_2_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Tofauti na somo la Historia, akiolojia haichunguzi sana maandishi hasa ili kupata ufafanuzi wa mambo ya kale. Historia inatazama zaidi habari zilizoandikwa lakini akiolojia inatazama vitu vilivyobaki kutoka zamani. Wanaakiolojia wanaweza kutumia maandishi na habari za historia wakiamua jinsi gani waendelee na utafiti wao, kwa mfano wachimbe wapi. Lakini hutumia mitindo ya sayansi mbalimbali kuchunguza vitu vinavyopatikana kwa njia ya akiolojia.
20231101.sw_2_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Kinyume chake, matokeo ya akiolojia ni chanzo muhimu kwa wachunguzi wa historia. Mara nyingi matokeo ya akiolojia yanaweza kupinga au kuthibitisha habari zilizoandikwa au kufungua macho kwa kuzielewa tofauti.
20231101.sw_2_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Mfano bora wa akiolojia ni utafiti wa mji wa Pompei huko Italia. Habari za Pompei zimepatikana katika maandishi mbalimbali ya Kiroma, lakini mji uliharibika kabisa na kufunikwa na majivu ya volkeno Vesuvio mwaka 79 B.K.
20231101.sw_2_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Kuanzia mwaka 1748 wataalamu walianza kuchimba mahali pa mji mpotevu wakaupata. Hadi leo sehemu kubwa ya mji umefunuliwa tena. Chini ya majivu na udongo wa karne nyingi vitu vingi vimehifadhiwa vizuri ambavyo vingepotea kabisa visingefunikwa, kwa mfano picha za Kiroma zenye rangi nzuri kabisa kwenye kuta za nyumba. Hata mabaki ya chakula yamepatikana yakachunguzwa.
20231101.sw_2_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Ujuzi wa akiolojia ni muhimu sana kwa ajili ya historia ya Afrika. Tamaduni nyingi za Afrika ziliendela bila maandishi hadi juzi au hata leo. Habari zetu kuhusu utamaduni wa Zimbabwe Kuu au kuhusu uenezi wa Wabantu hutegemea akiolojia kwa kiasi kikubwa sana.
20231101.sw_2_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Akiolojia
Akiolojia
Hivyo akiolojia huongeza ujuzi wetu kwa kufunua ushahidi wa nyakati za kale; wakati huohuo kazi ya akiolojia inahatarisha ushahidi huo kwa sababu kazi yake huondoa hifadhi ya udongo. Katika karne za kwanza za akiolojia mabaki mengi ya tamaduni za kale yameharibika kutokana na kufunuliwa kwao. Kuepukana na tatizo hilo ni jukumu muhimu la akiolojia ya kisasa.
20231101.sw_10_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Daktari
Daktari
Daktari (au dokta; wingi wake unaundwa kwa kutanguliza ma-) ni neno lenye asili ya Kilatini ("doctor") lililoingia Kiswahili kwa kupitia Kiingereza. Hutumiwa kwa maana mbili:
20231101.sw_10_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Daktari
Daktari
1) Mtaalamu aliyepata mafunzo maalum kwenye chuo kikuu cha kutibu maradhi ya wagonjwa. Mtu wenye ujuzi wa kutibu anaitwa pia mganga (wa), tabibu (ma). Daktari humtibu mgonjwa kwa kutumia sindano, kumtundikia dripu n.k. baada ya kumpima baadhi ya vitu kama:
20231101.sw_10_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Daktari
Daktari
Kumpima mapigo ya moyo n.k. Maranyingi daktari hufanya kazi yake katika sehemu maalumu iitwayo Hospitali.
20231101.sw_10_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Daktari
Daktari
2) Kwa kufuata tabia za lugha nyingine daktari hutumiwa pia kama jina la heshima kwa mtu aliyepata shahada ya uzamivu au "PhD" ambayo ni shahada ya juu kabisa.
20231101.sw_16_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia
Historia
Historia (kutoka Kigiriki ιστορια, historia; pia "tarehe" kutoka Kiarabu تاریخ tarih kwa maana ya "historia": pia tena "mapisi") ni somo kuhusu maisha ya binadamu na utamaduni wao wakati uliopita.
20231101.sw_16_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia
Historia
Mara nyingi neno hilo lina pia maana ya maarifa yoyote kuhusu wakati uliopita, yawe au yasiwe maarifa ya watu (kwa mfano "historia ya ulimwengu").
20231101.sw_16_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia
Historia
Binadamu anaziandika ili kuelewa maisha yake, yaani ametokea wapi, amepata mafanikio gani na matatizo gani.
20231101.sw_16_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia
Historia
Historia inatufundisha kuishi: kumbukumbu za mambo ya zamani (vita, uhuru, viongozi na mengineyo) zinatuwezesha kuendelea vizuri zaidi.
20231101.sw_16_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia
Historia
Wanahistoria wanapata maarifa yao kutoka maandishi ya zamani (hasa kwa historia andishi), kutoka fasihi simulizi na kutoka akiolojia (hasa kwa historia ya awali).
20231101.sw_17_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Kwa ujumla, historia ni kumbukumbu ya maisha ya mwanadamu duniani, hasa ile tarehe iliyosajiliwa na kuhifadhiwa katika vitabu, maandishi mbalimbali, na simulizi au hekaya za mapokeo. Ingawa historia iliyobebwa katika simulizi na hekaya huchukuliwa na baadhi kuwa haina nguvu kwa kukosa ithbati ya maandishi, bado hivi ni vyanzo muhimu vya historia. Mara nyingi historia iliyoko katika maandishi huwa imehifadhiwa katika simulizi na hekaya kwa muda mrefu kabla ya kuandikwa.
20231101.sw_17_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Hapo kale, bara la Afrika lilishuhudia matukio mengi ya harakati za mwanadamu kuliko mabara mengine ya ulimwengu.
20231101.sw_17_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wataalamu wa athari wamegundua athari za zamadamu zinazorudi nyuma kufikia hadi miaka milioni minne, na athari za ustaarabu wa Wamisri wa Kale huko Misri na Wafoinike huko Tunis na sehemu nyinginezo za Afrika ya Kaskazini katika karne ya 9 KK.
20231101.sw_17_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Harakati za madola makubwa ya Warumi na Waarabu ziliweza kuonekana kabla ya karne ya 4 BK, na Waarabu walianza kuingia Afrika huko Habasha (Ethiopia) tangu karne ya 7 BK na kutangaza dini ya Uislamu na kuieneza katika maeneo mbalimbali ya Afrika pamoja na kuanzisha biashara na ustaarabu na kuimarisha mamlaka zao katika Sudan ya wakati huo tangu karne ya 8 baada ya Kikristo.
20231101.sw_17_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Himaya za Ghana, Mali, na Songhai zilikuwa zikijulikana kwa utajiri mkubwa na biashara stawi iliyokuwa ikifanyika wakati huo ya dhahabu na bidhaa nyinginezo. Mwisho wa karne ya 15 BK, himaya ya Songhai ilikuwa na nguvu kuweza kuitia chini ya utawala wake mamlaka ya Mali. Sehemu nyingine za kusini mwa Afrika zilikuwa wakati huu hazijulikani sana, na historia yake ilikuwa bado haijasajiliwa.
20231101.sw_17_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Baina ya karne ya 1 KK na karne ya 16 BK watu waliokuwa wakizungumza lugha ya Kibantu watokao sehemu za Nigeria na Cameroon ya leo, ndio waliokuwa wameenea kwenye sehemu mbalimbali kusini mwa bara la Afrika, wakiwa wameanzisha vijiji, mashamba na mamlaka katika sehemu za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya leo, za Luba na Mwememutapa, lakini makundi ya wachungaji wa wanyama walianza kuhamia kusini katika karne za 15 na 16 na kukutana na Wabantu. Ndipo walipoanzisha mamlaka zao za Bunyoro, Buganda, Rwanda na Ankole.
20231101.sw_17_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wazungu walianza kugundua bara la Afrika katika karne ya 15, wakati Wareno walipokuja kwenye fukwe za bara la Afrika kutafuta njia nyepesi na ya amani ya kufikia India, na kuweza kupata nafasi ya kushikilia biashara ya dhahabu na pembe na watumwa ambayo ilikuwa ikiendelea wakati huo katika bara la Afrika. Katika mwaka 1488 Bartolomeo Dias alizunguka Rasi ya Tumaini Jema (kwa Kiingereza: Cape of Good Hope), na katika mwaka 1498 Vasco da Gama alifika ufukwe wa Afrika Mashariki na kuendelea mpaka India.
20231101.sw_17_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Baada ya hapo, Ureno ulianzisha vituo vya biashara Afrika, ukifuatiwa na Waholanzi, Waingereza, Wafaransa na Wazungu wengineo, na biashara ya watumwa iliyosimamiwa na Waarabu na baadhi ya Waafrika wenyewe ikashika kani na kuwa na kasi na nguvu.
20231101.sw_17_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wakati huohuo Waturuki walishikilia sehemu za kaskazini ya Afrika na Waomani wakashikilia ufukwe wa Afrika Mashariki.
20231101.sw_17_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Kati ya miaka 1880 na 1912, Wazungu waligawana bara la Afrika, na nchi zote zikawa chini ya utawala wa Wazungu isipokuwa Liberia na Ethiopia.
20231101.sw_17_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wafaransa wakachukuwa Afrika Magharibi na Kaskazini na kwa hivyo nchi za Afrika Magharibi: Dahomey (sasa Benin), Guinea, Mali, Cote d'Ivoire, Mauritania, Niger, Senegal na Volta ya Juu (sasa Burkina Faso) zilikuwa chini ya utawala wake. Hali kadhalika, Algeria, Tunisia na Morocco zilitawaliwa na wao. Aidha, Wafaransa walitawala Togoland, Somaliland, Madagascar, Comoro, na Reunion.
20231101.sw_17_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Waingereza nao wakatawala Afrika Mashariki na Kusini, na kuwa sehemu ya Sudan na Somalia, Uganda, Kenya, Tanzania (chini ya jina la Tanganyika), Zanzibar, Nyasaland, Rhodesia, Bechuanaland, Basutoland na Swaziland chini ya utawala wao na baada ya kushinda katika vita huko Afrika ya Kusini walitawala Transvaal, Orange Free State, Cape Colony na Natal, na huko Afrika ya Magharibi walitawala Gambia, Sierra Leone, the Gold Coast na Nigeria.
20231101.sw_17_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wareno wakachukuwa sehemu ya Guinea, Angola na Msumbiji na sehemu na visiwa fulanifulani huko Afrika ya Magharibi.
20231101.sw_17_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wabelgiji wakachukua Kongo na Rwanda-Urundi, na Wahispania wakachukua sehemu ya Guinea, Spanish Sahara (sasa Sahara ya Magharibi), Ifni na sehemu nyingine za Morocco.
20231101.sw_17_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Wajerumani nao wakachukua Togoland, Cameroon na baadhi ya nchi katika Afrika ya Magharibi na Afrika ya Mashariki, lakini baada ya vita vya kwanza vya dunia wakanyang'anywa.
20231101.sw_17_15
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Nchi ya kwanza kujitawala upya katika Afrika ni nchi za Afrika ya Kusini zilizojiunga na kujiendesha wao wenyewe katika mwaka 1910. Misri, katika mwaka wa 1922 walikuwa wanajiendesha wenyewe, na Tangier katika mwaka wa 1925.
20231101.sw_17_16
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Madola mengi ya Afrika yalianza kupigania uhuru katika miaka ya baina ya 1950 na 1960, na Wazungu wakasalimu amri na kuanza kutoa uhuru. Libya wakajinyakulia uhuru katika mwaka wa 1951, Eritrea katika mwaka 1952 ikiwa imejiunga na Ethiopia, Morocco katika mwaka wa 1956, na wakarudishiwa Tangier.
20231101.sw_17_17
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Katika mwaka huu wa 1956, Sudan na Tunisia vile vile walipata uhuru wao, na Ghana katika mwaka wa 1957, Guinea katika mwaka wa 1958, na vile vile Morocco wakarudishiwa Spanish Morocco.
20231101.sw_17_18
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Katika mwaka wa 1960 Ufaransa ukatoa uhuru kwa Cameroon, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Chad, Congo (Brazzaville), Cote d'Ivoire, Dahomey (Benin), Gabon, Madagascar, Mali, Mauritania, Niger, Senegal na Volta ya Juu (Burkina Faso).
20231101.sw_17_19
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Vile vile, katika mwaka huohuo wa 1960 Congo (Kinshasa), Nigeria, Somalia, na Togo zikapata uhuru, na katika mwaka wa 1961 Sierra Leone na Tanganyika zikapata uhuru, na Afrika ya Kusini ikawa Jamhuri.
20231101.sw_17_20
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Katika mwaka wa 1962 Algeria, Burundi, Rwanda, na Uganda zikawa huru, na 1963 zikafuatia Zanzibar, Gambia na Kenya, na katika mwaka wa 1964 Malawi (Nyasaland), na Zambia (Rhodesia ya Kaskazini) zikapata uhuru.
20231101.sw_17_21
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Baada ya miaka miwili, katika mwaka wa 1966 Botswana (Bechuanaland) na Lesotho (Basutoland) zikajinyakulia uhuru. Mauritius na Swaziland katika mwaka wa 1968 na vile vile Guinea ya Ikweta. Hispania ikairudisha Ifni katika mwaka wa 1969 katika mamlaka ya Morocco.
20231101.sw_17_22
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Aidha, katika mwaka wa 1974 Guinea ya Kireno (Guinea-Bissau) ikapata uhuru wake, na katika mwaka wa 1975 Angola, Cape Verde, Mozambique, Sao Tome na Principe zikapata uhuru. Hispania vilevile ikaitoa Sahara ya Magharibi kwa Morocco na Mauritania katika mwaka wa 1976, lakini wananchi wakakataa kuwa chini ya nchi mbili hizi, kukazuka vita. Mauritania ukaitoa sehemu yake na kuipa Morocco katika mwaka wa 1979, tatizo ambalo mpaka sasa linaendelea baina ya Morocco na Sahara ya Magharibi, na Umoja wa Mataifa unajaribu kutatua tatizo hili. Waingereza wakawapa uhuru Shelisheli katika mwaka wa 1976, na Ufaransa ukatoa uhuru kwa visiwa vya Ngazija (Comoro).
20231101.sw_17_23
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Katika mwaka wa 1977 Jibuti (Nchi ya Afars na Issas) iliyokuwa ikitawaliwa na Wafaransa ikarudi kwa wenyewe. Rhodesia (Zimbabwe) ikapata uhuru halisi mwaka wa 1980, na South West Africa, iliyokuwa ikitawaliwa na Afrika ya Kusini ikapata uhuru katika mwaka 1990 na kuitwa Namibia.
20231101.sw_17_24
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Uingereza umebaki na visiwa vya Saint Helena na Ascension, na Ufaransa unaendelea kutawala Mayotte na Reunion. Hispania vilevile unaendelea kutawala visiwa vya Canarias pamoja na Ceuta na Melilla na visiwa viwili vingine vilivyoko karibu na Morocco.
20231101.sw_17_25
https://sw.wikipedia.org/wiki/Historia%20ya%20Afrika
Historia ya Afrika
Korotayev A. & Khaltourina D. Introduction to Social Macrodynamics: Secular Cycles and Millennial Trends in Africa. Moscow: URSS, 2006. ISBN 5-484-00560-4 .
20231101.sw_20_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Hesabu
Hesabu
Hesabu (afadhali: Hisabati kutoka neno la Kiarabu vilevile) ni somo linalohusika na idadi na jinsi tunavyoweza kuhesabu kwa kutumia hasa kanuni zifuatazo: kujumlisha, kutoa, kuzidisha na kugawa n.k.
20231101.sw_24_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jiografia
Jiografia
Neno la Kiswahili jiografia linafuata matamshi ya Kiingereza ya neno la Kigiriki "γεωγραφία", geo-grafia kutoka gê "dunia" na graphein "kuandika". Lina maana ya "kuandika kuhusu Dunia". Neno hili lilianza kutumiwa kwa mara ya kwanza na mwanasayansi Eratosthenes (276-194 KK).
20231101.sw_24_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Jiografia
Jiografia
Sehemu za jiografia ni vitu kama mabara, bahari, mito na milima. Wakazi wake ni watu wote na wanyama waishio juu yake. Maajabu yake ni vitu vinavyotokea kama vile maji kujaa na kupwa, upepo, na tetemeko la ardhi.
20231101.sw_30_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Kiesperanto ni lugha ya kupangwa inayozungumzwa zaidi duniani kati ya lugha hizi. Ilipangwa na Ludwik Lejzer Zamenhof, myahudi aliyetoka mjini Białystok, nchini Urusi (siku hizi ni sehemu ya nchi ya Poland). Alitoa kitabu cha kwanza cha lugha hii mwaka 1887 baada ya kuitengeneza kwa miaka karibu kumi. Nia yake ilikuwa kutengeneza lugha rahisi ili iwe lugha saidizi ya kimataifa, lugha ya pili kwa kila mtu duniani. Waesperanto wengine bado wanataka hiyo, lakini wengine wanapenda kuitumia tu bila nia ya kuieneza duniani kote.
20231101.sw_30_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Waesperanto wanakitumia Kiesperanto kwa ajili ya kukutana na wageni na kujifunza kuhusu nchi na tamaduni nyingine. Siku hizi, maelfu ya watu wanaitumia mara kwa mara ili kuwasiliana na watu popote duniani.
20231101.sw_30_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Chunguzi za kitaalamu zimeonyesha kwamba Kiesperanto kinaweza kujifunzwa rahisi zaidi sana kuliko lugha asilia, na pia kwamba kujifunza Kiesperanto kwanza kunarahisisha kujifunza kwa lugha nyingine.
20231101.sw_30_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Kwa kuwa lugha ya kupangwa, Kiesperanto hakiko katika familia yoyote a lugha. Maneno yake yanatoka hasa lugha za Kirumi (kama Kifaransa na Kilatini), lakini pia lugha za Kigermaniki (kama Kiingereza na Kijerumani) na lugha za Kislavoni (kama Kirusi na Kipolandi). Maneno mengi yanaumbwa kwa kuunganisha mzizi wa neno moja na viambishi au kwa kuunganisha mizizi ya maneno mbalimbali. Kwa mfano kuna kiambishi awali "mal-" inayoonyesha kinyume: "bona" ni "-zuri" na "malbona" ni "-baya". Kwa hiyo inawezekana kusema mambo mengi baada ya kujifunza maneno machache tu.
20231101.sw_30_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Katika Kiesperanto kuna harufi 28 na kuna sauti 28. Kila harufi inaweza kutamka kwa sauti moja tu, na kila sauti inaandikwa kwa serufi moja tu. Harufi za Kiesperanto ni zifuatazo:
20231101.sw_30_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Kwa upande wa konsonanti, b, d, f, g, h, k, l, m, n, p, r, s, t, v na z zinatamka kama kwa Kiswahili. c inatamka kama ts. ĉ inatamka kama ch. Matamshi ya ĝ yanafanana na matamshi ya j kwa Kiswahili (ni sawasawa na matamshi ya j katika neno la Kiswahili "njia"); j ya Kiesperanto inatamka kama y ya Kiswahili. ĵ inatamka kama j ya Kifaransa (inafanana na sh ya Kiswahili, lakini inatamka na sauti, kama z). ŝ inatamka kama sh. ŭ inatamka kama w; ŭ inatumika baada ya a na e tu, ingawa Zamenhof wenyewe na Waesperanto wengine waiunganisha na irabu yoyote, k.m. "sŭahila" (Kiswahili), "ŭato" (wati), tena jina la herufi yenyewe ni "ŭo"; tofauti kati ya au na aŭ ni kwamba au inatamka kwa silabi mbili na aŭ kwa silabi moja.
20231101.sw_30_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Nomino (majina) zote zinahitimu kwa kiambishi tawali -o, kwa mfano "arbo" (mti). Wingi wa nomino unahitimu kwa -oj (arboj = miti).
20231101.sw_30_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Kiesperanto
Kiesperanto
Vivumishi vinahitimu kwa kiambishi tawali -a, kwa mfano "alta" (-refu). Vivumishi kwa kawaida vinawekwa kabla ya nomino inayohusu, lakini pia inaweza kuwa baada yake. Wingi pia unaonyeshwa katika vivumishi kwa harufi "j": altaj arboj = miti mirefu.
20231101.sw_31_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20ya%20kuundwa
Lugha ya kuundwa
Lugha ya kuundwa (au lugha unde) ni lugha ambayo misamiati na sarufi zake zimetungwa na watu badala ya kukua kama sehemu ya utamaduni wa umma fulani. Kwa kawaida zinaundwa kwa ajili ya kuwasiliana kati ya watu sawasawa na lugha asilia. Nyingi zinatengenezwa ili kuwa lugha saidizi za kimataifa, lakini nyingine zinaundwa kwa ajili ya usiri au majaribio ya isimu au bila sababu fulani.
20231101.sw_31_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20ya%20kuundwa
Lugha ya kuundwa
Mara chache lugha ya kuundwa maana yake ni lugha za kompyuta au za kuandaa programu (angalia lugha asilia). Kwa sababu ya utata huo watu wengi, hasa Waesperanto, hawapendi kutumia neno lugha ya kuundwa, na badala yake wanasema lugha ya kupangwa. Msemo lugha ya kupangwa unatumika kwa lugha zile tu ambazo ziliundwa kwa ajili ya utumiaji wa kawaida baina ya watu, kama Kiesperanto.
20231101.sw_31_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20ya%20kuundwa
Lugha ya kuundwa
Mfano mwingine wa lugha ya kuundwa ni lugha ya sheng' inayozungumzwa nchini Kenya hasa miongoni mwa vijana. Lugha hiyo Haina wazawa asilia mahali popote ila tu ilizuka miongoni mwa vijana Kwa kutaka kusitiri mazungumzo Yao. Hivi ni kuunga mkono wazo la hapo awali kwamba lugha unde Huwa Kwa Sababu za kusitiri mazungumzo au kuunda programu za kompyuta kama vile lugha iitwaya "binary language" ambayo hutumika katika vifaa vya kielektroniki Ili kuundia programu zake. Lugha hiyo ndio hueleweka na mashine za kielektroniki kama tarakilishi au kikokotoo.
20231101.sw_32_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha (kutoka neno la Kiarabu: لغة) ni utaratibu wa kuwasiliana kati ya binadamu (wengine wanadai hata kati ya viumbe wenye akili).
20231101.sw_32_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zenye maana na zilizokubaliwa na jamii ya watu fulani ili zitumike katika kuleta mawasiliano.
20231101.sw_32_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu kwa sababu zilitokea kama bahati tu kwa binadamu. Wanyama hawatumii lugha kama chombo cha mawasiliano, kwa kuwa lugha ni sauti zenye maana na kukubaliwa na jamii.
20231101.sw_32_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Hakuna lugha bora zaidi duniani, kwa kuwa lugha zote zina ubora, mradi zikidhi matakwa ya jamii husika.
20231101.sw_32_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Mbali na maana ya kawaida kuna pia lugha ya ishara inayotumiwa na watu bubu. Katika fani ya programu za kompyuta ni kawaida kuongea juu ya "lugha ya kompyuta".
20231101.sw_32_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha hukua: lugha hukua (kuongezeka kwa maneno, kuongezeka kwa idadi ya wazungumzaji, kuwa na mawanda mapana, kusanifiwa) kadiri inavyoendelea kutumiwa na jamii.
20231101.sw_32_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha hufundishika: mtu yeyote anaweza kujifunza walau kiasi lugha yoyote hata kwa njia ya ufundishaji.
20231101.sw_32_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha lazima ijitosheleze: kila lugha inajitosheleza kulingana na mahitaji ya jamii inayotumia lugha yenyewe.
20231101.sw_32_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha hufa: inapozidi mno kubadilika mwisho si yenyewe tena, lakini pia inapoachwa isitumike tena kwa kuwa wahusika wanapendelea lugha nyingine.
20231101.sw_32_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Lugha huwa na mpangilio maalumu wenye kubeba maana. Mpangilio huo huanza na fonimu ---> Silabi ---> Neno
20231101.sw_32_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Hii ni lugha ambayo huwasilishwa na watu kwa njia ya mazungumzo ya mdomo - na hurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mazungumzo. Lugha ya mazungumzo ni kongwe, hai na halisi zaidi ya mzungumzaji na ina maana nyingi, kwani mzungumzaji na msikilizaji huwa ana kwa ana katika mazingira mamoja.
20231101.sw_32_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Hii ni lugha ambayo huwasilishwa kwa njia ya maandishi. Hii ni kiwakilishi cha lugha ya mazungumzo katika mfumo wa maandishi. Lugha ya maandishi ni changa kwani imeanza milenia za hivi karibuni baada ya kuvumbuliwa kwa maandishi.
20231101.sw_32_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Kwa kawaida, lugha ni sehemu ya utamaduni wa umma fulani. Lugha ya aina hii inaitwa lugha asilia. Lakini pia kuna lugha za kuundwa.
20231101.sw_32_13
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Tangu siku za kwanza za binadamu, lugha zimekuwa zikichipuka, kukua, kutangaa na kufa kama kiumbe yeyote mwingine. Kwa hivyo, lugha zilizopo leo ulimwenguni, huenda baada ya karne nyingi kupita zikatoweka na kuzuka nyinginezo.
20231101.sw_32_14
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha
Lugha
Leo ulimwenguni mathalan, kuna lugha karibu 6,700, zikiwa 1,000 katika bara la kaskazini na la kusini la Amerika, 2,000 zikiwa kwenye bara la Afrika, 230 katika bara la Ulaya, 2,200 katika bara la Asia, na 1,300 katika bara la Oshania (Australia na nchi jirani nayo).
20231101.sw_33_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20asilia
Lugha asilia
Lugha asilia ni lugha ambayo ilikua kama sehemu ya utamaduni wa umma fulani ambao watu wake wanaiongea kama lugha mama. Ni kinyume cha lugha ya kuundwa (lughaundwe).
20231101.sw_33_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20asilia
Lugha asilia
Mara nyingine lugha asilia maana yake ni lugha yoyote ambayo inaweza kuzungumzwa na watu, huku lugha za kompyuta na za kuandaa programu zinaitwa lugha za kuundwa.
20231101.sw_33_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Lugha%20asilia
Lugha asilia
Mara nyingine tena lugha asilia ni lugha ambayo mtu huzaliwa nayo au huikuta baada ya kuzaliwa. Hata hivyo lugha asilia huwa chimbuko la watu fulani katika jamii na hutofautisha jamii moja na nyingine. Mara nyingi ni sehemu ndogo tu ya jamii ndiyo huwa na lugha asilia yaani kila ukoo au kabila huwa na lugha yake ya asili.
20231101.sw_65_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madola
Madola
Katika mabara, lile lenye nchi nyingi zaidi ni Afrika likiwa na nchi au madola 54, likifuatiwa na bara la Ulaya likiwa na madola 48, kisha Asia likiwa na madola 44, halafu Amerika ya Kaskazini pamoja na Amerika ya Kati likiwa na madola 23, na baada yake ni Australia na Pasifiki (Oshania) likiwa na madola 14, na mwishowe ni Amerika ya Kusini likiwa na madola 12. Kwa hivyo, kwa ujumla, kuna madola 195 ulimwenguni.
20231101.sw_65_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Madola
Madola
(AS)= Asia (AF)= Afrika (NA)= Amerika ya kaskazini (SA)= Amerika ya kusini (A)= Antaktika (EU)= Ulaya na (AU)= Australia na nchi za Pasifiki.
20231101.sw_71_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Sayansi ni maarifa yanayopatikana kwa kufanya vitendo, kutazama na kujaribu kweli ambazo zimebainishwa hazijathibitishwa.
20231101.sw_71_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Msingi wa sayansi ni vitendo. Vitendo vya kisayansi vina njia zake zinazotumika kuthibitisha kweli fulani.
20231101.sw_71_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Namna ya kueleza jambo kisayansi huchimbuka toka nadharia ama udhanifu. Halafu, ili kweli ikubalike, hutoka kwenye udhanifu na kwa kupitia majaribio rasmi, hutengeneza dhana kamili ama nadharia kama ni shauri la kueleza mwenendo na tabia.
20231101.sw_71_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Hivyo, asili ya njia ya kisayansi ni mtazamo unaokwenda sambamba na vitendo vinavyochunguzwa. Kutoka mitazamo wanasayansi wanaunda nadharia. Baadaye wanaangalia kama bashiri za nadharia ni kweli. Zisipokuwa kweli watakanusha nadharia hiyo. Ikionekana kwamba mara nyingi sana nadharia ilibashiri ukweli, na haijakosea, itakuwa nadharia inayokubalika.
20231101.sw_71_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Mara chache, maarifa yatokanayo na sayansi yanaweza kupinga hali ya kawaida. Kwa mfano nadharia ya atomu inasema kwamba katika jiwe (maada yabisi) kuna uvungu (dutu tupu), na kwamba atomi zinacheza katika nafasi ndogo katika jiwe ukifananisha na maada kimiminika. Lakini kwa nadharia hii tunaweza kueleza mambo mengi, hata kwa nini tunaweza kusema kwamba jiwe halina uvungu.
20231101.sw_71_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Sayansi iliaanza kama udadisi wa mtu mmojammoja; lakini kadiri maarifa yanavyopanuka, inakuwa vigumu kwa mtu mmoja kufanya mchango wa kujitenga. Hivyo jumuiya zimebeba kusudi ambalo hapo mwanzo lilionekana kama ni shauku la mtu mmojammoja kama awali.
20231101.sw_71_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Hii hufanya mkururo wa ugunduzi ama uvumbuzi kuwa sehemu ya historia ya sayansi. Majina na sifa hutajwa sambamba na shauri la aliyepelekea.
20231101.sw_71_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Sayansi na jamii huenda pamoja katika kuleta mabadiliko, kwa kuwa mabadiliko huletwa na watu wenyewe.
20231101.sw_71_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Katika dunia hii ya leo, maendeleo ya watu hujidhihirisha sana kutokana na jinsi jamii husika ilivyopiga teke katika uwanja huu.
20231101.sw_71_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Ingawaje haibainishwi wazi miongoni mwa sura ya mambo ya kidunia, sayansi kwa kweli ni nguvu inayoweza kubadili maisha ya watu kwa wema; lakini katika kilele chake cha mafanikio, vyombo vyenye nguvu za mamlaka na fedha hushikilia baadhi ya matunda yake katika hali ya kibiashara na kiutawala zaidi.
20231101.sw_71_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sayansi
Sayansi
Wapo watu pia ambao hutumia sayansi kujaribu kuboresha maisha ya watu wote kwa ujumla. Hivyo sayansi haibakii tu mikononi mwa wenye kushika dau kimifumo, bali changamoto ya wote wenye kutaka kuleta maendeleo ya ujumla.
20231101.sw_72_0
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza law ) ni mfumo wa kanuni, ambazo kwa kawaida hutekelezwa kupitia seti ya taasisi maalumu. Inaunda siasa, uchumi na jamii kwa njia mbalimbali na huratibu mahusiano baina ya watu.
20231101.sw_72_1
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya mali inafafanua haki na wajibu unaohusiana na uhamisho wa jina la mali ya binafsi na mali ya kweli.
20231101.sw_72_2
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya hifadhi inatumika kwa mali yanayotumika kwa uwekezaji na usalama wa kifedha, huku sheria ya kukiuka wajibu inaruhusu madai ya fidia ikiwa haki au mali za mtu zinafanyiwa madhara.
20231101.sw_72_3
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Ikiwa madhara ni kinyume cha sheria, sheria ya jinai inatoa mbinu zinazoweza kutumiwa na taifa ili kumshtaki mhusika.
20231101.sw_72_4
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya kikatiba inatoa utaratibu wa utungaji wa sheria, ulinzi wa haki za kibinadamu na uchaguzi wa wawakilishi wa kisiasa.
20231101.sw_72_5
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya utawala inatumika kuangalia upya maamuzi ya vyombo vya serikali, huku sheria ya kimataifa inatawala shughuli baina ya nchi huru zinazohusu mambo kama vile biashara, vikwazo vya kimazingira na hatua za kijeshi.
20231101.sw_72_6
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Akiandika mnamo 350 K.K., mwanafalsafa wa Ugiriki ya Kale Aristotle alisema, "Utawala wa sheria ni bora kuliko utawala wa mtu yeyote binafsi."
20231101.sw_72_7
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Mifumo ya sheria inaelezea haki na majukumu kwa njia mbalimbali. Tofauti ya jumla inaweza kufanywa kati ya maeneo yanayotawaliwa na mfumo wa sheria ya kiraia, ambayo huandika sheria zao, na yale yanayofuata sheria za kawaida, ambapo sheria haijaundwa kwa utaratibu maalumu. Katika baadhi ya nchi, sheria ya dini bado hutumika kama sheria maalum. Sheria ni chanzo kikuu cha uchunguzi wa kitaalam, wa historia ya sheria, falsafa ya sheria, uchambuzi wa kiuchumi wa sheria au somo la kijamii kuhusu sheria.
20231101.sw_72_8
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria pia huibua masuala muhimu na magumu kuhusu usawa, uadilifu na haki. "Katika usawa wake wa ajabu", alisema mwandishi Anatole France mnamo mwaka 1894, "sheria inakataza matajiri na mafukura kulala chini ya madaraja, kuombaomba barabarani na kuiba mikate." Katika demokrasia ya kawaida, taasisi za msingi za kutafsiri na kuunda sheria ni matawi matatu makuu ya utawala, ambayo ni mahakama isiyo na upendeleo, bunge na serikali yenye kuwajibika.
20231101.sw_72_9
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Ili kutekeleza na kutumia nguvu za kufanya sheria ifuatwe na kutoa huduma kwa umma, urasimu wa serikali, jeshi na polisi ni muhimu. Vyombo hivyo vyote vya dola viliundwa na kutawaliwa na sheria, taaluma ya kisheria iliyo huru na jamii yenye bidii zinajulisha na kusaidia maendeleo.
20231101.sw_72_10
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Mifumo yote ya kisheria inahusu na masuala ya msingi, lakini kila taifa inaainisha na kubainisha masomo yake ya kisheria kwa njia mbalimbali. Tofauti ya kawaida ni kuwa "sheria ya umma" (maneno yanayohusika kwa karibu na taifa, na kuhusisha sheria ya kikatiba, kitawala na ya jinai), na "sheria ya kibinafsi" (inayohusisha mkataba, sheria ya kukiuka wajibu na mali). Katikamifumo ya sheria ya kirai , mkataba na kukiuka wajibu zinapatikana chini ya sheria ya majukumu huku sheria ya hifadhi inapatikana chini ya serkali za halali au mikataba ya kimataifa. Sheria ya Kimataifa, kikatiba, kitawala, jinai, mkataba, kukiuka wajibu na mali na hifadhi zinatambulika kama "masomo msingi ya jadi", ingawa kuna masomo zaidi ambayo yanaweza kuwa na umuhimu mkubwa zaidi wa kiutendaji.
20231101.sw_72_11
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya kimataifa inaweza kuashiria mambo matatu: sheria ya umma ya kimataifa, sheria ya kibinafsi ya kimataifa au mgongano wa sheria na sheria ya mashirika makubwa ya kimataifa.
20231101.sw_72_12
https://sw.wikipedia.org/wiki/Sheria
Sheria
Sheria ya Umma ya Kimataifa inajihusisha na uhusiano kati ya mataifa uhuru. Vyanzo vya maendeleo ya sheria ya umma ya kimataifa ni desturi, mwenendo na mikataba kati ya nchi huru Mikataba ya Geneva. Sheria ya umma ya kimataifa inaweza kutengezwa na mashirika ya kimataifa, kama vile Umoja wa Mataifa (ambao ilianzishwa baada ya kushindwa kwa Shirikisho la Kimataifa kuzuia Vita vya Vikuu vya Pili vya Dunia), Shirika la Kimataifa la Ajira, Shirika la Kimataifa la Biashara, au Shirika la Fedha la Kimataifa. Sheria ya kimatifa ya umma ina hadhi maalum kama sheria kwa sababu hakuna kikozi cha kimataifa cha polisi, na mahakama (kama vile Mahakama ya Kimataifa ya Haki kama tawi la kimsingi la Umoja wa Mataifa la mahakama) halina uwezo wa kuadhibu kutokutii. Hata hivyo, miili michache, kama vile WTO, ina mifumo yenye ufanisi ya utatuzi wa kudumu na utatuzi wa mogogoro inayoambatana na vikwazo vya kibiashara.
README.md exists but content is empty. Use the Edit dataset card button to edit it.
Downloads last month
0
Edit dataset card